Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali
AG FELESHI AWASHUKURU SAMIA NA JPM
service image

Na Mwandishi Maalum

14/7/2022

Dodoma

Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Feleshi, ameishukuru Serikali  kwa  uamuzi wake  wa kuijumuisha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali    pamoja na Wizara ambazo zimepewa fedha za  kujenga Majengo ya  Kudumu  katika Mji wa Serikali wa Mtumba,   Jijini  Dodoma.

Ametoa shukrani  hizo leo, alhamisi, wakati alipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa  Jengo jipya  la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika mji  huo wa wa Serikali.

“Ninawashukuru sana  Maraisi   kwa maono yao na utambuzi wao  wa  kuiunganisha  Ofisi  ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali   na Wizara mbalimbali   katika awamu ya kwanza na ya pili  ya  ujenzi wa majengo  ya kudumu hapa Mtumba.  Hii ni heshima kubwa kwetu na  hasa kwa kuzingatia  unyeti wa majukumu yetu”. Akaeleza Mhe. AG

Katika ziara yake hiyo fupi na ambayo alikuwa ameambatana na  Menejimenti yake,  AG Feleshi amesema uamuzi wa Serikali  wa kuwa na majengo ya kudumu ya serikali katika Mji wa Serikali wa Mtumba ni uamuzi wa kihistoria kwa vizazi na vizazi na umeufanya mji huo wa Serikali kuwa kivutio cha kitalii.

“ Majengo haya ni ya kudumu, ni historia kwa  vizazi na  vizani  na  kwa miaka mingi ijayo.  Kwa  hiyo  nyinyi wakandarasi ambao mmepata fursa ya  kujenga majengo haya lazima mjivunie historia hii kwa kufanya kazi wa uadilifu na kwa  wakati, kwa sababu mnaandika historia”. amesisitiza  AG Feleshi

 Jengo  la Ofisi  ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  lenye ghorofa tano  na   umbo la herufi Y  linajengwa na   Mkandarasi SUMA JKT  Kanda ya Kati kwa gharama ya . Licha  ya kuwa na umbo la herufi Y, litakapokamilika  litakuwa ni  kati ya majengo makubwa  matatu  katika majengo yote ya serikali  yanayojengwa katika mji huo wa serikali  pia ni  moja     ya majengo makubwa  matatu    katika  majengo yote ya serikali yanayoendelea kujengwa katika mji huo wa Serikali.

AG Feleshi pamoja na kuridhishwa na  namna kazi ya jenzi wa  mradi huo unaotarajiwa kugharimu  ....... mpaka  kukamilika kwake  amemtaka Mkandarasi kutosita kumpatia  taarifa endapo  kutakuwa na  uchelewesashi  wowote au urasimu  kutoka pande zote mbili ( mteja na   mkandarasi) ili aweze kuchukua hatua zozote.

“Mmenieleza hapa kwamba kwa sasa hamna changamoto kubwa,  ila niwaombe  kama kutakuwa   na changamoto yoyote iwe kutoka Ofisini kwangu au kutoka Jeshini  msisite kunijulisha ili hatua za mapema zichukuliwe. Lakini sisi ni wasimamizi wa Sheria, pia nisingependa kuona kunajitokeza matatizo yoyote ya kisheria kwenye mradi huu”.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali pia alijiridhisha kwamba fedha za utekelezaji wa mradi huo zimekuwa zikitolewa kwa wakati kila  Mkandarasi anapowasilisha  hati zake ( Certificate) na kwamba hakuna malimbilizo yoyote.

Awali akitoka maelezo ya maendeleo ya  mradi huo  Mshauri  Mwelekezi Mhandisi  William Sele  kutoka  Wakala wa  Majengo ( TBA) alimweleza Mhe. AG na Ujumbe wake kwamba kazi ya ujenzi wa jengo hilo  unakwenda vizuri kwa asilimia 26 ya ujenzi na kwamba  hawategemei kupata changamoto  kubwa labda uhaba wa mali ghafi  hapo baadaye.

Mhandisi Sele pia amesema  sasa hivi  TBA  inajitahidi sana katika  usimamizi wa kazi zake ili kwenda na wakati na kuondoa malalamiko  ya kwamba TBA wamekuwa  wakishelewesha utekelezaji  na ukamilishaji wa miradi mbalimbali.

“Sasa hivi kwa kweli  tumejipanga  vizuri,  kazi zinakwenda kwa wakati,  vibali vinatolewa kwa wakati, huko nyuma TBA tulikuwa tunalalamikiwa  kwa ucheleweshaji wa vibali na mengineyo kama hayo, sasa tupo vizuri”, akasema  Mhandisi Sele.

mwisho

 

14 Jul, 2022
Maoni