Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali
KUTOKA VIWANJA VYA NYERERE ( NYERERE SQUARE)DODOMA
service image

Na Mwandishi wetu

23/01/2022

Maonesho  ya Utoaji wa Huduma za Kisheria na Msaada wa kisheria yameingia katika siku yake ya pili ambapo  Banda la   Ofisi  ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  limepokea wananchi wa kada mbalimbali  waliofika  kupata huduma za ushauri na  msaada wa kisheria.

Maonesho  haya   yameandaliwa na  Mahakama ya Tanzania ikiwa ni  sehemu ya uzinduzi wa mwaka  mpya wa Mahakama mwaka ambao  utazinduliwa rasmi February Mosi 2023 katika Viwanja vya  Chinangali.

Leo  (jumatatu) Jaji kiongozi  Mhe. Mustapher Siyani leo alitembelea baadhi ya mabanda na  kupewa  taarifa mbalimbali  kutoka kwa wahudumu wa mabanda  hayo  naye  alitoka  maagizo kadhaa.

Wateja ambao  wanatembelea Banda la OMMS kupata huduma  wamekuwa wakiomba kupewa ushauri  na masaada wa kisheria katika maeneo mbalimbali  yakiwamo  maswala ya  ajira,  hukumu zilizotolewa na  mahakama, na wengine wakiitaka Ofisi ya Mwanasheria  Mkuu wa Serikali  kuangalia uwezekano  wa Kwenda  maeneo ya nje  ya Jiji la Dodoma ili kutoa elimu ya sheria na  msaada wa kisheria  kwa wananchi walioko maeneo ya vijijini.

Ujumbe wa mwaka huu  ni  Umuhimu wa Utatuzi wa Migogoro kwa Njia ya Usuluhishi katika Kukuza Uchumi Endelevu Wajibu wa Mahakama na Wadau.

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  kama mdau wa mahakama  katika kuutekeleza kwa vitendo ujumbe huo,  Mwaka 2020 OMMS ilitoa mwongozo maalumu ambao ulizishauri  na  kuzitaka Taasisi za Serikali   zinapoingia  kwenye migogoro zitumie njia za usuluhishi kwanza, chini ya usimamizi wa  Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa  Serikali   badala ya kukimbilia mahakamani .

 Mawakili wa Serikali wanohudumu  katika Banda hili ni  Angela Kimaro,  Hery Sanga na  Sindeyan Suyaani.

Imeandaliwa Kitengo cha Mawasiliano

 

23 Jan, 2023
Maoni