Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali
OFISI YA MWASHASHERIA MKUU WA SERIKALI YAPATIWA VIFAA VYA TEHEMA
service image

OFISI YA MWASHASHERIA MKUU WA SERIKALI  YAPATIWA VIFAA VYA TEHEMA

Na  Mwandishi Maalum

Makampuni ya  Supperdoll na Kagera Sugar   yametoa vifaa vya kisasa vya TEHAMA ikiwa ni  kuunga mkono jitihada za Serikali  na hususani  Ofisi ya   Mwanasheria Mkuu wa Serikali  za  kuimarisha na kuboresha  utekelezaji wa  majukumu yake kupitia mawasiliano ya kisasa ya   TEHAMA.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni hayo Bw. Seif Ally Seif  akiongozana  viongozi wengine kutoka makampuni hayo jana ( Jumatatu)   alimkabidhi   Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Mhe. Jaji Dk. Eliezer Feleshi, Komputa za kisasa za mezani  5 ( Desktop), Komputa mpakato za kisasa 5 ( laptop) na Printa ya kisasa  moja katika hafla   fupi iliyofanyika  jijini  Dodoma.

Kupatikana  kwa  vifaa hivyo kuna tokana na  mazungumzo ya awali yaliyowahi kufanyika kati ya  AG Feleshi na uongozi  wa Makampuni hayo ambapo  AG pamoja na  mambo mengine alielezea  mweleko wa Ofisi yake na hamu  kubwa  ya kuona Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali inakuwa na vifaa vya kisasa vya Tehama na  ndipo  Uongozi wa Makapuni hayo  ulipoahidi  kusaidia.

Akikabidhi  vifaa hivyo, Bwa. Seif Ally Seif alimweleza   AG  Feleshi kwamba,  Makampuni yake yataendelea kushirikiana  na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Serikali kwa ujumla kwa kadri ya uwezo  wake.

Akipokea vifaa hivyo,  AG   Feleshi akiwa  na  viongozi wengine  kutoka Ofisi yake,  pamoja na kushukuru kwa msaada huo. Amesema,  Ofisi  itahakikisha  inavitumia  vifaa hivyo kwa malengo yaliyokusudiwa  kwa kuwahudumia  wadau wake ndani ya  serikali na nje ya serikali kwa weledi na kwa wakati.

Aidha  AG  Feleshi  ameahidi kuwa  Ofisi yake itaendelea kushirikiana kwa karibu na wadau wake wote.

28/6/2022

28 Jun, 2022
Maoni