Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali
VIONGOZI WA TUGHE TAWI LA OFISI YA MWANASHERIA MKUU WAASWA KUWA WAADILIFU
service image

Na Mwandishi  Maalum

Dodoma

15/11/2022

Viongozi wa  Chama  cha Wafanyakazi (TUGHE) Tawi la  Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  wameaswa  kuwa waamini na waadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao.

Rai hiyo  imetolewa leo ( Jumanne ) na  Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Dkt. Evaristo Longopa wakati akifungua mafunzo ya siku  moja ya wanachama wa TUGHE tawi la  ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

 Mafunzo hayo yametolewa na  viongozi wa Tughe Mkoa wa Dodoma   na kufanyika   katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya  Mwanasheria Mkuu  Mtumba,  Jijini Dodoma.

“Nitoe rai kwenu viongozi wa TUGHE  muonyeshe  uadilifu na uaminifu ili  wanachama wenu wawe na imani kwenu lakini  pia wajue michango  yao  inatumikaje tumikaje , je  inatumika vizuri na kwa manufaa yao?” akasema na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Akaeleza pia  kuwa, kwa viongozi kuonyesha uadilifu na uaminifu kutawafanya wanachama waliopo  waendelee kukipenda chama  chao, lakini  uandilifu huo na uaminifu utawavutia  wanachama wapya.

Akizungumzia kuhusu   mafunzo  nayo,  Dkt. Longopa ameelezea  kufurahishwa  kwake   na mafunzo  hayo  ambayo  ameyataja kuwa ni muhimu kwa wanachama kwani  yatawawezesha kuwa na uelewa wa Pamoja kuhusu  chama chao. 

Akasema   Chama cha Wafanyakazi  sehemu ya kazi ni chambo muhimu sana hasa katika kutetea haki,  maslahi na maendeleo   ya wafanyakazi.

Ni kwa sababu hiyo, amewataka viongozi hao wa TUGHE  tawi la  OMMS  kuhakikisha wanaongeza jitihada za kuwahamasisha wanachama  wapya hasa wale ambao  hawana vikwanzo vya kisheria kujiunga.

“ Wafanya kazi   wengi bado hawafahamu  manufaa na faida za kujiunga na TUGHE, mwanachama anapopata  shida mahali  pakazi  na pale menejimenti inapotaka  kumpatia adhabu,  TUGHE mahali pa  kazi huwa wanakuwa na mchango mkubwa wa kumterea  mfanyakazi yule na  mara nyingi   TUGHE imekuwa ikiwasaidia sana wanachama sehemu ya  kazi” akasisisita DAG .

Akaongeza kuwa  inakuwa rahisi sana kwake kukutana na uongozi wa TUGHE  kwa niaba ya wafanyakazi badala ya kukutana  na mfanyakazi mmoja moja, kwa hiyo    wafanyakazi watambue  umuhimu na nafasi ya  TUGHE katika kutetea maslahi  na haki zao  kwa kujiunga na  TUGHE.

Mkufunzi Mkuu wa Mafunzo hayo ambaye ni    Katibu  TUGHE Mkoa ( Dodoma) Bw. Samuel Nyungwa   pamoja na kuelezea chimbuko  la TUGHE pia alisisitiza haja na umuhimu kwa viongozi  kuwa na   uwazi hasa katika masuala ya fedha kwa kutoa  taarifa sahihi.

Bw. Samuel Nyungwa pia  katika mafunzo amefafanua haja na umuhimu  wa TUGHE tawi la  OMMS kuwa  daraja la mawasiliano na maridhiano  baina ya wafanyakazi  na Menejimenti.

Akabainisha kwamba inapokuja suala la kutetea maslahi , haki na maendeleo ya wafanyakazi, Viongozi wa TUGHE  wanawajibika  kuwakilisha makundi yote bila ya  kubagua.

Bw. Nyungwa amezitaja nguzo tatu  muhimu  za TUGHE ambazo ni   umoja wa wanachama,  uhuru na demokrasia.

 Mada ambazo nzime tolewa katika  Mafunzo hayo ni Pamoja umuhimu wa chama cha wafanyakazi mahali pa kazi, na  namna  bora ya uendeshaji wa chama ili wanachama  washiriki kikamilifu katika chama chao mada iliyotolewa na  Afisa Elimu TUGHE Nsubisi Mwasandende na  namna bora ya kuwa na  mahusiano mazuri  na  menejimenti

Awali akimkaribisha mgeni rasmi kufungua  mafunzo hayo ,  Katibu wa TUGHE tawi la  OMMS Bi, Dorina Kalumuna amesema  kwa sasa TUGHE  Tawi la OMMS linawachama  54.

Pamoja  wanachama wa  TUGHE kushiriki mafunzo   hayo,  wengine walioalikuwa  kushiriki walikuwa ni wajumbe wawakilishi kutoka Divisheni na Vitengo vya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali .

Na Mwandishi  Maalum

Dodoma

15/11/2022

Viongozi wa  Chama  cha Wafanyakazi (TUGHE) Tawi la  Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  wameaswa  kuwa waamini na waadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao.

Rai hiyo  imetolewa leo ( Jumanne ) na  Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Dkt. Evaristo Longopa wakati akifungua mafunzo ya siku  moja ya wanachama wa TUGHE tawi la  ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

 Mafunzo hayo yametolewa na  viongozi wa Tughe Mkoa wa Dodoma   na kufanyika   katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya  Mwanasheria Mkuu  Mtumba,  Jijini Dodoma.

“Nitoe rai kwenu viongozi wa TUGHE  muonyeshe  uadilifu na uaminifu ili  wanachama wenu wawe na imani kwenu lakini  pia wajue michango  yao  inatumikaje tumikaje , je  inatumika vizuri na kwa manufaa yao?” akasema na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Akaeleza pia  kuwa, kwa viongozi kuonyesha uadilifu na uaminifu kutawafanya wanachama waliopo  waendelee kukipenda chama  chao, lakini  uandilifu huo na uaminifu utawavutia  wanachama wapya.

Akizungumzia kuhusu   mafunzo  nayo,  Dkt. Longopa ameelezea  kufurahishwa  kwake   na mafunzo  hayo  ambayo  ameyataja kuwa ni muhimu kwa wanachama kwani  yatawawezesha kuwa na uelewa wa Pamoja kuhusu  chama chao. 

Akasema   Chama cha Wafanyakazi  sehemu ya kazi ni chambo muhimu sana hasa katika kutetea haki,  maslahi na maendeleo   ya wafanyakazi.

Ni kwa sababu hiyo, amewataka viongozi hao wa TUGHE  tawi la  OMMS  kuhakikisha wanaongeza jitihada za kuwahamasisha wanachama  wapya hasa wale ambao  hawana vikwanzo vya kisheria kujiunga.

“ Wafanya kazi   wengi bado hawafahamu  manufaa na faida za kujiunga na TUGHE, mwanachama anapopata  shida mahali  pakazi  na pale menejimenti inapotaka  kumpatia adhabu,  TUGHE mahali pa  kazi huwa wanakuwa na mchango mkubwa wa kumterea  mfanyakazi yule na  mara nyingi   TUGHE imekuwa ikiwasaidia sana wanachama sehemu ya  kazi” akasisisita DAG .

Akaongeza kuwa  inakuwa rahisi sana kwake kukutana na uongozi wa TUGHE  kwa niaba ya wafanyakazi badala ya kukutana  na mfanyakazi mmoja moja, kwa hiyo    wafanyakazi watambue  umuhimu na nafasi ya  TUGHE katika kutetea maslahi  na haki zao  kwa kujiunga na  TUGHE.

Mkufunzi Mkuu wa Mafunzo hayo ambaye ni    Katibu  TUGHE Mkoa ( Dodoma) Bw. Samuel Nyungwa   pamoja na kuelezea chimbuko  la TUGHE pia alisisitiza haja na umuhimu kwa viongozi  kuwa na   uwazi hasa katika masuala ya fedha kwa kutoa  taarifa sahihi.

Bw. Samuel Nyungwa pia  katika mafunzo amefafanua haja na umuhimu  wa TUGHE tawi la  OMMS kuwa  daraja la mawasiliano na maridhiano  baina ya wafanyakazi  na Menejimenti.

Akabainisha kwamba inapokuja suala la kutetea maslahi , haki na maendeleo ya wafanyakazi, Viongozi wa TUGHE  wanawajibika  kuwakilisha makundi yote bila ya  kubagua.

Bw. Nyungwa amezitaja nguzo tatu  muhimu  za TUGHE ambazo ni   umoja wa wanachama,  uhuru na demokrasia.

 Mada ambazo nzime tolewa katika  Mafunzo hayo ni Pamoja umuhimu wa chama cha wafanyakazi mahali pa kazi, na  namna  bora ya uendeshaji wa chama ili wanachama  washiriki kikamilifu katika chama chao mada iliyotolewa na  Afisa Elimu TUGHE Nsubisi Mwasandende na  namna bora ya kuwa na  mahusiano mazuri  na  menejimenti

Awali akimkaribisha mgeni rasmi kufungua  mafunzo hayo ,  Katibu wa TUGHE tawi la  OMMS Bi, Dorina Kalumuna amesema  kwa sasa TUGHE  Tawi la OMMS linawachama  54.

Pamoja  wanachama wa  TUGHE kushiriki mafunzo   hayo,  wengine walioalikuwa  kushiriki walikuwa ni wajumbe wawakilishi kutoka Divisheni na Vitengo vya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali .

 

15 Nov, 2022
Maoni