Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali
WATUMISHI OMMS WAPATIWA SEMINA KUHUSU AFYA YA AKILI SEHEMU YA KAZI
service image

Na  Mwandishi wetu

Mtumba-Katika miaka ya hivi  karibuni   pamekuwapo  na   taarifa  kutoka vyanzo mbalimbali vinavyoelezea ongezeko la  changamoto  zinatokana na afya  ya  akili au msongo wa Mawazo.

Matatizo hayo mawili  yamekuwa yakiwakumba watu wa kada tofauti tofauti wakiwamo  wafanyakazi.

Ingawa  hakuna  twakimu sahihi lakini  hakuna ubishi kwamba tatizo la au changamoto ya afya ya akili  na msongo wa Mawazo  ni kati ya magonjwa ambayo  si ya kuambukiza lakini  yanayochangia kwa kiasi kikubwa maendeleo  na utendaji kazi kwa idadi kubwa ya  watu.

Katika kutambua  uwepo wa changamoto hiyo, Divisheni ya Uratibu na  Huduma za Ushauri wa  Kisheria(DCAS)  Alhamisi  Septemba 22,2023  iliandaa  mafunzo ya siku moja  kuhusu  Afya ya Akili  kwa Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Mafunzo hayo  yalifanyika katika  ukumbi wa  Mikutano Mtumba Jijini Dodoma

Semina  au mafunzo  hayo kuhusu  suala la afya  ya akili mahali  pa kazi  yalitolewa na  Dkt. Garvin Nathaniel Kweka kutoka   Hospitali ya Taifa ya  Muhimbili ambaye pia ni Daktari mbomezi wa  ya magonjwa  ya Figo.

Akimkaribisha  mtalaam huyo  Mkurugenzi wa Divisheni ya Uratibu na Huduma za Ushauri wa Kisheria  Dkt. Gift Kweka,  alisema, Divisheni yake iliamua kuratibu semina hiyo   hasa   kwa kuzingatia  uzito na aina ya  majukumu yanayotekelezwa  na    watumishi wa OMMS majukumu ambayo kwayo ndani yake  yana  stress  nyingi.

“tumeona kuna haja  na umuhimu tukapata  semina au mafunzo haya kuhusu afya ya akili ili    yatusaidie   sisi kama  watumishi wa OMMS   kuweza kuweka  uwiano mzuri katika utekelezaji wa majukumu yetu na namna  bora ya kukabiliana na  stress  zinazotokana na majukumu hayo ili  kwa ujumla itusaidie kutekeleza majukumu yetu kwa ufanisi na tija lakini  kama watu binafsi  tuwe na afya  bora ya  akili”. Akasema  Mkurugenzi  Kweka.

Semina au  mafunzo hayo  yalihudhuriwa  pia na Mkurugenzi wa Divisheni ya Utawala na  Raslimali   Watu Bw. Silas Marwa, na  Watumishi kutoka  Divisheni nyingine ikiwamo  Divisheni  iliyoratibu  mafunzo hayo (DCAS)

 

22 Sep, 2023
Maoni